Ilipoishia “Aaaah Zola” ilisikika sauti upande wa Mzee Dawson, ikioneshaย alikuwa akijigeuza.ย
“Hebu fanya taratibu tuonane ana kwa ana Mzee Dawson, nahisiย kuchanganikiwa sasa” Zola alikata simu bila kusikiliza sautiย ya Mzee Dawson, baada ya hapo akapiga simu sehemu nyingineย ndani ya kitengo cha siri cha Mzee Dawson kinachoitwa MPA,ย akaomba madaktari waweze kufika eneo la tukio, akawapa Ramaniย kamili lilipo eneo hilo.ย Endelea
SEHEMU YA NNE
Hakuwa na muda wa kukaa pale, akatoka taratibu hadi nje,ย akayaangalia vizuri mazingira yale kwa jicho na akili yaย kipelelezi akajua tu kifo kile kimetokea masaa machacheย yaliyopita na kwa vyovyote mwenye chumba kilichokuwaย kinaangaliana na mlango lilikofanyika tukio atakuwa labdaย amesikia au kuona chochote kile, akakumbuka kuwa mlango huoย ulifungwa na funguo kuondolewa, akajiuliza haraka akiwaย analitazama dirisha la Chumba jiraniย
“Kama funguo imetolewa maana yake kuna Mtu amefunga mlango naย kumfungia Mtu ndani, Nani amefanya hivi?” Akapata akili yaย kusogea chumba cha jirani, alipogonga akatoka yule Msichanaย ambaye alimuelekeza chumbani kwa Anastanzia, yule Mdadaย alipomuona Zola akaanza kujishebedua kwa kuhisi kuwa Zolaย alikuwa akimtaka, alionekana kuvutiwa na Mzee Zola kutokanaย na muonekana wa kitajiri alionao bila kujuwa kuwa alikuwaย amesimama mbele ya Mtu hatari kwa upeleleziย
“Nilijua tu utakuja kwangu, Anastanzia sio aina ya Mwanamkeย ambaye anakufaa wewe. Wazee kama nyie mnatakiwa kupetiwaย vizuri ili msiwe na mawazo ya kufa kufa” Alisema hukuย akitabasamu mbele ya Zola, kisha Zola akamuuliza yuleย msichana
“Mara ya mwisho umemuona Anastanzia lini?” Mdada akaachaย kujishebedua baada ya Zola kuonesha sura ya mbuziย
“Wiki sasa sijamuona ila rafiki yake si umeonana nae? Maanaย nimekuona ukitoka humo ndani” Zola akatoa kitambulisho chaย uaskari akamuonesha yule mdada kisha akamuulizaย
“Unaitwa nani?” Mdada akawa anatetemekaย
“Naitwa Scolastica”ย
“Rafiki yake Anastanzia amekufa, naomba uniambie ni naniย umemuona akiingia au kutoka mle ndani kabla yangu Mimi”ย
“Kulikuwa na Mkaka mmoja hivi, aliingia kisha akafunga mlangoย akatoka, sikumuona tena”ย
“Anafananaje?”ย
“Mrefu kiasi, mweusi ana rasta”ย
“Sikia, watakuja polisi kuchukua mwili wa Marehemu, asanteย kwa ushirikiano wako” Zola akaingia kwenye gari yakeย akatokomea eneo hilo, akawasiliana na Mzee Dawson ili wapateย kukutana na kuzungumza, Mzee Dawson kama kawaida yakeย akamueleza Zola wakutane sehemu ya siri.ย
Alipofika Zola, Mzee Dawson aligundua ni jinsi gani Zolaย alikuwa katika nyakati ngumu ambayo hakupata kumuona nayo,ย akamimina mvinyo kwenye glasi na kumpatia, akapiga funda mojaย la mvinyo ukawa umeisha kwenye Glasi, kisha akaitua Glasiย hiyo mezani kama Mtu aliyechoshwa na kinachoendelea.ย
“Dawson! Hili jambo ni zito sana, kulifahamu lilipo kundi laย Mafia Gang, na kuwajua Watu hao inakuwa kazi ngumu sana.ย Sijui ni mafunzo ya namna gani watu hao wanapatiwa kabla yaย kutekeleza jambo fulani” Alisema Zola huku akakunja midomoย yake, akampa Glasi Mzee Dawson ili amuongeze mvinyo,ย ukamiminwa mvinyo kwenye Glasi ya Zola haraka kisha Dawsonย akakaa vizuri ili amjibu Zola, kwanza akajikoholesha kishaย akasemaย
“Mauwaji yaliyofanywa na Mafia Gang huko Congo yanatishaย sana, hapa bado kabisa hawajavuruga kisawasawa! John Brainย kama lilivyo jina lake ni Mzungu hatari sana Zola, nahisiย yupo hapa Nchini na kuna mpango wanautekeleza, umejaribuย kufuatilia ni mafaili gani yaliibiwa na huyo Msichana katikaย kituo cha polisi” Zola alitikisa kichwa kuashiriaย hakufuatilia suala hilo, Dawson akapiga tena fundo la Mvinyoย kisha akabeua kidogo
“Zola ninayemjua Mimi hawezi kukosa kujuwa mambo kama hayo,ย akili yako haipo kabisa Zola, John Brain ana akili sana naย anachezea ubongo wako! Huenda ameshakujua na kukufuatilia,ย anachofanya ni kukuchezesha, hapa kuna mambo mawili huendaย yanafanyika kwa wakati mmoja”ย
“Mambo gani hayo?”ย
“Wananunua Muda wako na muda wa Wapelelezi wengine iliย watekeleze mipango yao, hata haya mauwaji yanayotokea huwendaย wanakuhadaa ili usipate muda wa kutuliza akili yako, wanajuwaย wewe ni hatari kiasi gani, hilo lipo wazi Zola”ย
“Hili suala linaninyima usingizi Dawson, nahisi nipo katikaย chumba chenye giza ambacho siwezi kuona kuna nini ndani yakeย hata kusikia sauti inayonipa ishara, nahisi kushindwa”ย
“Ha!ha!ha! Zola, huwezi kukata tamaa mapema hivi, umekulaย kiapo cha kulinda Taifa hili ikiwemo kupambana na Watu ainaย ya John Brain, nafikiri muda unaenda, umekuja na gari yako?”ย
“Ndio”ย
“Tuitumie sasa hivi”ย
“Tunaenda wapi?” Aliuliza Zola huku akimtazama kwa makiniย Mzee Dawson ambaye tayali alionekana kuwa ameshaanza kulewaย lakini alimjuwa sawa sawa jinsi alivyo, akilewa huwa anaamuwaย mambo kwa kutumia akili sana.ย
“Tunaenda Hospitali kuruhusu ile Maiti moja iliyosalia kwendaย kuzikwa”ย
“Tutawapa vipi Maiti ambayo si yao, kumbuka ile ni Maiti yaย Anastanzia na sio Sandra”ย
“Tunairudisha sura ya Bandia kama ilivyo Mwanzo, huu sioย wakati wa wao kujuwa ukweli, acha waamini wanamzika Mtu wao”ย Waliitumia gari ya Zola hadi walipofika Hospitali, tayariย maiti mbili zilikuwa zimeruhusiwa kwenda kwa wahusika ambazoย ni Maiti ya Bosco na Robert.ย
Wakasimamia zoezi la kuveshwa sura kwa Mwili wa Anastanzia,ย dakika chache muonekano ulibadirika,ย
“Yes! Acha wamzike wanayemuamini huku sisi tukiwa bizeย kufuatilia” Alisema Dawson kisha alikohoa kama kawaida yake,ย Zola akampa kitambaa akawema mdomoni lakini alipokitoaย ilionekana damu katika kitambaa hicho cheupe kuashiria kuwaย mapafu ya Mzee Dawson yalikuwa katika hali mbaya
“Usijali” akasema Dawson, kisha Zola akapiga simu kwenyeย familia ya Mama Sandra ili waende kuuchukuwa mwili walioaminiย ni wa Sandra ili wakauzike.ย
“Naingia kazini sasa Zola, tuna muda mchache sana kuhakikishaย Nchi inakuwa shwari” alisema Dawson na kumfanya Zolaย atabasamu maana mzigo ulikuwa ukimuelemea sana. Sikuย iliyofuata Mazishi ya Sandra yalifanyika, Zola alikuwaย miongoni mwa waliohudhuria lakini uwepo wa Zola msibaniย ulikuwa na melengo makuu mawili, moja kuhakikisha familiaย haitambui kama anayezikwa si Sandra, jambo la pili aliaminiย kama Mpango ule ulisukwa basi wasukaji wangefika pale Msibaniย kwa ajili ya kufuatilia, lakini Pia Zola alimtilia shaka Babaย yake Sandra akiamini anajuwa jambo fulani.ย
Akiwa ameketi alivalia miwani nyeusi na sura ya Bandia kamaย alivyoambiwa na Mzee Dawson kuwa Huenda Mafia Gangย wameshamjuwa ndio maana walitaka kumuuwa katika jaribio laย bomu, hakutambuliwa na yeyote pale lakini alionekana kuwaย miongoni mwa waliokuja Msibani, Watu walikuwa wengi mno. Kifoย kile kilishika mioyo ya wengi.ย
Naam!! Zola alikuwa bize sana kuhakikisha anazungusha machoย yake kila kona, macho yake yakajikuta yametua kwa jamaa mmojaย ambaye naye alikuwa bize sana kuzungusha macho yake, Zolaย hakufanikiwa kugundulika baada ya kubadilisha sura kishaย kuvaa miwani, ingehitaji utaalam mkubwa sana kumtambua.ย Kilikuwa ni kipindi ambacho Msemaji wa Familia alikuwaย akiwashukuru Watu waliokuja pale kwa ajili ya maziko yaย Sandra ambaye alizikwa pale pale nyumbani kwao, Zola hapoย ndipo akajithibitishia kuwa familia ya Sandra haikusanukaย kuwa walikuwa wakizika Maiti ya Mtu mwingine, lakini hakusitaย kukubali uwezo wa Maadui zao ambao walifanikiwa kuuhadaaย ulimwengu wa vipofu ambao macho yao hayakuweza kuona mbaliย zaidi ya Jicho la kipelelezi lenye mafunzo ya kijeshi ambaloย Zola alikuwa nalo.ย
Kwa mantiki hiyo, Maadui walifanya tafiti zao kabla yaย kumtumia Anastanzia kuvaa sura ya Sandra maana miili yaoย ilifanana sana ndio maana hawakuweza kuhisi kama kuna tatizo,ย akashusha pumzi zake, alijuwa ilitumika akili kubwa sana paleย hadi Anastanzia akaingizwa kwenye mwanvuli ule wa Umauti,ย swali lililomjia akilini mwake haraka ni wapi alipo Sandraย mwenyewe?. Aliporejesha macho eneo la yule jamaa aliyekuwaย akimfuatilia, aliona kiti kikiwa kitupu kabisa, akaangazaย huku na kule bila mafanikio yoyote ndipo akaona ni bora atokeย nje ili apeleleze yule jamaa ni nani na kwanini alikuwaย akichezesha yale macho ya kipelelezi, akamkubuka sawasawaย jamaa huyo mwenye upara na ndevu nyingi.
Alinyanyuka kutoka kitini kama Mtu aliyemaliza tukio laย mazishi, hakutaka kuonesha dalili zozote kuwa alikuwaย akifuatilia chochote maana aliamini Maadui walikuwepo paleย Msibani, akiwa anatoka aligongana na Mwanamke mmoja mrefu,ย mweupe na mwenye nywele nyingi.ย
“Samahani?” Alisema Mwanamke huyo ambaye alikuwa na uzuri waย kutosha, macho ya Zola yakautalii mwili wa Mwanamke huyo bilaย staraย
“Usijali!” Akasema Zola kisha akatoka pale taratibu bilaย kugeuka nyuma.ย
Yule Mwanamke alimtazama sana Zola hadi alipozama, kishaย akaketi kitini. Zola alipofika nje alimuona yule jamaaย akizungumza na simu kisha akaingia kwenye gari, Zolaย hakuchelewa naye akaingia kwenye gari na kuanza kumfuatiliaย jamaa huyo ambaye alionekana kutokuwa na wasiwasi wowote uleย maana hata alivyoendesha gari hilo ilionesha wazi kuwaย alikuwa katika hali ya kawaida, akaingia Barabara ya tanoย kisha akashika barabara kuu ambayo ilikuwa ikitoka Uwanja waย ndege kuelekea eneo ambalo lilikuwa na Hoteli nyingi za nyotaย tano.ย
Bila kupoteza muda Zola alimpigia Dawson simu, akamuelezaย hali ilivyo kisha akasubiria jibu la Mzee huyo.ย
“Washa GPS ya Gari” ilisikika sauti kutoka upande wa pili,ย ikampa ishara Zola kuwa Mzee Dawson alikuwa na maelekezoย maalum ya nini cha kufanya.ย
“Nakuona!” Alisema Dawson kisha alikata simu mara moja, baadaย ya dakika tano akampigia tena na kumwambiaย
“Fuata maelekezo yangu, kuwa makini hao Watu wana akili yaย ziada sana wakati mwingine Watu hawaamini kama Huyo Mzungu niย Binadamu, wana akili iliyozidi…unaweza kuwa umetegwa, kablaย ya kutoka Msibani hakuna ishara tata?” Alimpa wakati waย kufikria, Zola akasemaย
“Nilikuwa makini kuliko kawaida, hakuna aliyeniona ila wakatiย natoka…” Ukimya ukatawala, Mzee Dawson akamuuliza Zolaย
“Enhee ilikuwaje?” Zola akafikiria alipokuwa akitoka paleย aliparamiana na Mwanamke mmoja mzuri sana, hakutaka kulisemaย hilo akiamini sio ishara ya kumueleza Mzee Dawsonย
“Sio ishara!”ย
Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TANOย USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kupiga Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย
ย Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx ย Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx ย Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx ย Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx
9 Comments
Ukalii umepamba moto
Jasusi anajasusiwa. Noma sana
Aiseeeee hatar
โ๏ธโ๏ธ
Thank a lot, kazi nzuri
Iko poa xnaaa
Zola!ยก!!
Ni ๐ฅ๐ฅ๐ฅ๐ฅ๐ฅ๐ฅ
ZOLA AKIWA KAZINI