Ilipoishia “Inawezekanaje Zola?”
“Hiyo ndio hali halisi ndio maana nimekuita hapa iliย tuzungumze, nahisia mbaya juu ya Mkuu wa Nchi lakini sitakiย kujiaminisha chochote”ย
“Unataka kusema Mkuu wa Nchi kuna kitu anakificha hapa?” Woteย waliacha kunywa pombe wakazama katika maongezi yaoย Endeleaย
SEHEMU YA SITA
“Kama hausiki kwanini atoe amri kwa jeshi la polisi? Kwaniniย Mtuhumiwa afungwe katika Gereza lililopo Ikulu?” Alihoji Zolaย huku Dawson akionesha kuanza kuvuta picha ya maelezo ya Zola.ย
“Mimi nafikiria kwasasa tujikite zaidi na upelelezi kuhusuย Mafia Gang, hili jambo tuliweke kiporo Zola” Alisema Mzeeย Dawson, ni wazi kilichomfanya akae kimya kwa muda mrefuย kilikuwa ni hicho.ย
“Wewe ni mwalimu mzuri sana Dawson, kuliacha hili jambo niย sawa na kumega Mkate alafu ukajiaminisha kuwa hakunaย kilichotoka, umefundisha vijana wengi masuala ya upelelezi naย Ujasusi, sidhani hata hicho unachokizungumza kinatoka katikaย akili yako, sitaki kuamini pia kuwa pombe imekuingia kiasiย hicho. Ili tuukate huu mti ni lazima tukubali kung’oa miziziย ya Mti wenyewe ili usichipue tena”ย
“Zola tunaanzia wapi kumpeleleza Mkuu wa Nchi ambaye ndiyeย ametupa kazi hii, kama hili kundi lina maslahi kwake kwaniniย ameagiza tulifyeke? Nachelea kusema anaweza kuwa hausikiย hapa” Alisema Dawson huku macho yake madogo kama ya pakaย yaking’aza huku na kule, pombe ilikuwa ikishuka kwenye kooย lake lenye koromeo kubwa, kisha alibakuaย
“Ni bora kuachana na kazi hii Dawson kuliko kuruhusu dosaliย kwenye upelelezi huu, nimeweka Maisha yangu rehani, mwenyeweย umeona nilitaka kuuawa kama sio wewe kuwahi kuniokoa,ย tukubaliane hapa kuwa Rais apelelezwe kuhusu Mfungwaย aliyefungwa magereza ya Ikulu” Ulikuwa ndio msimamo wa Zola,ย Dawson alimuamini sana Zola akamwambiaย
“Kama ni hivyo basi uwanja ni wako Zola, siku ukithibitishaย kuwa Rais anahusika na Mauwaji haya utanijulisha,” Ilikuwaย ndio kauli ya mwisho ya Dawson, umri wake ulionesha ni jinsiย gani alikuwa akipambana na akili za uzee alizonazo licha yaย kuwa ni Mtu aliyeaminiwa sana na Idara ya Usalama wa Taifa,ย akamuaga Zola huku akimuachia ujumbe kuwaย
“Wakati unawatafuta wao wapo macho wanakutafuta” Alisemaย kisha alijizoa na kuondoka pale kwa kutumia gari yake yaย kifahari, licha ya uzee lakini alimudu kuliendesha mwenyewe.ย Muda huo mvua ilikuwa ikinyesha, Zola akawa anamtazama Dawsonย kupitia dirisha la kioo, Mzee Dawson alikuwa fundi waย kuendesha gari jambo lililomchekesha Zola akajikuta akisemaย
“Ng’ombe huyu amegoma kuzee Maini yake” Akarudi kuketi hukuย akizidi kutafakari, akamkubuka rafiki yake Mmoja aliyeitwaย Sande Olise aliyekuwa uhamishoni Nchini Botswana,ย alipomkumbuka alijikuta akitabasamu kisha akaenda ukutaniย ambapo kulikuwa na picha waliyopiga pamoja.ย
Sande Olise alikuwa ni miongoni mwa Wanafunzi waliopelekwaย Nchini Mexico kujifunza masuala ya upelelezi, Sandeย alipishana umri wa miaka saba na Zola, tabia zao za kupendaย wanawake ndizo zilizowafanya wakafahamiana, akakumbuka Jinsiย walivyopigana vita vya kukiokoa kisiwa kimoja kilichopo Njeย kidogo ya Mji Mkuu, kisiwa hicho kilivamiwa na Waasi kutokaย Nchi jirani na kukiweka chini ya Ulinzi kwa zaidi ya sikuย saba.ย
Zola alikaa chini akafikiria kumpigia simu Sande Olise,ย alipekuwa baadhi ya nyaraka fulani akakuta namba ya Sandeย kisha akampigia huku akitabasamu. Simu ilipokelewa huku sautiย nzito ilisikika upande wa piliย
“P045 Olise! Kuna mpango maalum?” Alichofanya Zola alipigaย simu ya Sande kwa kutumia namba maalum za siri, Wapeleleziย wote walikuwa na simu za siri hivyo Sande alipoona simu hiyoย alijuwa kulikuwa na shida mahali, japo sauti yake ilioneshaย kuwa alikuwa ameamshwa na simu ya Zola lakini alikaza sautiย yakeย
“P102 Zola! Over..” Alisema Zolaย
“Over!! Zola, za miaka mingi rafiki yangu” Alisema Sandeย Olise huku ile sauti ya ukakamavu ikiwa imetoweka baada yaย kugundua aliyekuwa akimpigia alikuwa ni rafiki yake kipenzi,ย Mafunzo waliyoyapokea huko Mexico waliambiwa kitu pekeeย wanachotakiwa kukiepuka ni urafiki sababu usaliti wa Nchiย huanza kirafiki hatimaye kuwa janga la Taifa, hivyoย waliheshimu misingi hiyo, ndiyo sababu ya kukaa Miaka mingiย bila kuwasiliana.ย
“Nzuri ndugu yangu Sande, upo wapi siku hizi?” Alihoji Zola “Nipo Botswana uhamishoni, nina kitengo cha siri huku”ย
“Pole kwa majukumu! Ulisikia juu ya kifo cha Makam wa Rais naย Matukio yanayoendelea huku?”
“Nimesikia Zola, najua Mtaalam wa kazi utakuwa upo mzigoni,ย lakini hao mnaopambana nao sijui kama ni saizi yenu, walikujaย huku Miaka mitatu iliyopita lakini balaa lake ni kubwa sana,ย wameuwa makomando 50, na taarifa nyingine zimefichwa”ย Yalikuwa ni maelezo ya Sande Oliseย
“Sande hali ni tete sana, hili jambo ni zito na hawa jamaaย wana mtandao Mkubwa sana Duniani, kupambana nao ni sawa naย kutupa jiwe gizani, wanauwa kama hawana akili nzuri”ย
“Ha!ha!ha!” Alicheka Sandeย
“Mbona unacheka Sande”ย
“Hao jamaa wanamafunzo maalum nasikia Mkuu wao anaitwa Johnย Brain, huyo Brain ndiyo mwalimu wa Osama Bin Laden,ย anajihusisha pia na Alqaeda…Ni ngumu kumtambua kwa sura ilaย alama kubwa ni vidole viwili wanavyoviacha wakiwa wamefanyaย mauwaji, Mimi nipo Uhamishoni, majukumu yamepungua nakulaย bata tuu sababu Mimi huku ni Bosi” Alisema Sande, lengo kuuย la Zola lilikuwa ni kumshawishi Sande arudi Nchini iliย washirikiane kupambana na Mafia Gang sababu Sande ni Mtuย pekee anayeweza kumuaminiย
“Sande lengo langu la kukupigia na kuhitaji msaada wakoย katika kazi hii ngumu niliyonayo, kuna uhusiano Mkubwa sanaย kati ya Rais wa Nchi na hawa Mafia Gang, ni hatari kwa sasa,ย siwezi kuinusa kwa pua zangu”ย
“Unataka nije kufa huko? CCP ina Wanafunzi wengi tulioendaย Mexico kipindi kile, ni Mimi tu Zola?”ย
“Hadi nakupigia wewe nina uhakika kazi hii tutaiweza kablaย mambo hayajaharibika zaidi, ujio wako utakuwa wa siri sanaย ili tupeleleze kwa kina ni jambo gani lipo nyuma ya kapeti”ย
“Ooh! Zola unajuwa siwezi kukukatalia, nitakujulisha nipeย siku tatu”ย
“Over!”ย
“Over!” Simu ilikatika mara moja, Zola akawa na tumaini laย Ujio wa Sande Olise ambaye waliwahi kumuita Duma wakimaanishaย ni Mtu mwenye kufanya mambo kwa haraka sana.ย
Zola akaelekea kitandani na kujipumzisha huku picha ya Raisย ikiwa katika macho na akili yake, alimuwazia Rais huyo. Akiwaย bado hajapata Usingizi Zola alipokea ujumbe wa simu kuwaย Askari aliyezungumza naye na kumpa taarifa juu ya Mfungwaย aliyefungwa katika Gereza la Ikulu ameuawa kwa kupigwa Risasiย akiwa ndani ya Kituo hicho, alishtuka kisha aliamka naย kuwasha taa, muda huo huo simu kutoka kwa Dawson iliingiaย
“Zola umeisikia hiyo taarifa?” Aliuliza Dawsonย
“Ndio nimeipata muda huu” Alijibu Zola kisha simu ilikatikaย
“Uuups!” Zola alivuta pumzi zake, taswira mbili zilimjia kwaย haraka haraka kuhusu mauwaji yale, upande mmoja ulimwambiaย kuwa Rais ndiye aliyekuwa akihusika na mauwaji yale lakiniย upande mwingine ulishindwa kumpa majibu ya kwanini Mafia Gangย wanafanya matukio yale, Kichwa chake kiliwaka moto.ย
Asubuhi mapema aliamka na kueleka kituo cha polisi, akakutaย hali ya huzunii ikiwa imetanda miongoni mwa polisi, Zolaย akauliza ni Nani aliyefanya Mauwaji yale, cha ajabu alikuwaย ni mmoja wa polisi ndiye aliyemuuwa yule polisi, Zolaย akashika kiuno chake kwa mshangao, akapelekwa alipohifadhiwaย Askari Muuwaji, hakutaka kuzungumza na Askari huyo akamwambiaย polisi mmoja amletee Mafaili ya kesi iliyowahusu Robert,ย Sandra na Bosco sababu ndio chanzo cha kuingizwa yeye katikaย majukumu yale mazito, akaondoka kituoni na kurudi katikaย Makazi yake ya siri, akayachoma moto mafaili hayo hukuย akiamini kuwa matukio yote yale yalifanywa kwa lengo laย kupumbaza jeshi la polisi ili wasijikite zaidi, walifanikiwaย kuwapoteza lakini Zola aliinusa hatari hiyo huku akijiulizaย Mafia Gang wanataka nini katika Nchi yao.ย
Muda huo huo Hekeheka ndani ya Kichwa Cha Zola iliongezeka,ย alijikuta akiwa katika hali ambayo ilihitaji matumizi makubwaย ya akili kuliko chochote kile. Kijasho chembamba kilikuwaย kikimtoka kwenye paji lake la uso, picha ya askari aliyeuawaย ilizunguka katika akili yake huku akijiuliza ni nani alitoaย maagizo ya Askari yule kuuawa, alijuwa fika kuwa askariย aliyemuuwa Askari mwenzake alishinikizwa kufanya hivyo, badoย aliamini Rais alikuwa mhusika namba moja wa mauwaji yale,ย akatoka nje huku akiwa anatazama taswira ya jua lilivyokuwaย likichangamsha bustani yake ndogo katika Makazi yake,ย pembezoni kulikuwa na njiwa waliokuwa wakiruka na kulia kwaย kupokezana.ย
Zola akaingia kwenye gari yake, akaelekea kituo cha polisi,ย safari hii alihitaji kumbana askari yule aliyemuuwa mwenzake,ย akaelekea chumba ambacho alihifadhiwa askari huyo kishaย akaomba polisi wote waondoke, wakabakia wawili tuu.ย
Zola alimtazama askari aliyekuwa akimtazama Zola kwa suraย kavu iliyojaa umakini, hakuonekana kujuta kwa kitendo kileย hata kidogo, Zola akamshika kichwa Askari huyo akamuuliza
“Nani amekuagiza umuuwe Askari mwenzako?” Aliuliza Zola hukuย akizidi kuvuta nywele za Askari huyo aliyefungwa pinguย mikononi kwa nyumaย
“Nani yupo nyuma ya tukio hili? Sababu najuwa huwezi kufanyaย hivi pasipo agizo maalum, huyu Askari alinieleza siriย aliyoijuwa….Nina imani hata wewe unaijuwa hiyo na ndiyoย sababu ya kumuuwa Askari mwenzako!!” Aliuliza tena Zola baadaย ya kuona swali la kwanza halikujibiwaย
“Fanya uliwezalo Zola, fanya tuu lakini siwezi kukwambiaย chochote zaidi tu ya kusema, nimemuuwa bila kuagizwa na Mtuย yeyote” Zola akachukua rungu la polisi akawa anampiga polisiย huyo sehemu za mbavu ili kuhakikisha anasema ni naniย aliyemtuma kufanya mauwaji ndani ya kituo hicho cha polisi.ย Askari huyo alikuwa akipiga kelele za maumivu, Zolaย aliendelea kumpiga hadi akawa anatema damu mdomoni, Zolaย alionekana kujawa na jazba sana. Muda huo simu yake iliita,ย ikawa auheni kwa Askari huyo ambaye alikuwa akipunguza sautiย ya kulalamika.ย
Zola akatupa lile rungu chini kisha akasogea ukutaniย akaipokea simu hiyo ambayo ilimfanya Zola kwanza awe mtii,ย mwenye kufuata maagizo, simu hiyo ilitoka ikulu, Zola alikuwaย akizungumza na Rais aliyeitwa Jacob Zagamba.ย
“Nakuja Mkuu” Alisema Zola kisha simu ilionekana kukatika,ย kijasho kilichokuwa kinamtoka Zola kilimwagika hadi kwenyeย singlendi yake nyeupeย
“Shiti!!” Akasema kisha akamtazama yule Askari ambaye alikuwaย akicheka kwa maumivu makali, Zola akachukua shati lake kishaย akaondoka pale mara moja. Safari hii Zola alikuwa akielekeaย Ikulu kuitika wito wa Rais wa Nchi hiyo, akiwa kwenye gariย akawasha Intaneti kisha akampigia simu ya Video Sande Oliseย aliyeko Botswana, bahati nzuri simu ilipokelewa haraka sanaย na Sande Oliseย
“Sande!! Mkuu wa Nchi ameniita, naelekea Ikulu sasa” Alisemaย Zola huku akiendelea kukanyaga mafuta kuelekea Ikulu.ย
“Nayaamini maneno yako, kuna mawili unaweza itiwa hapo, mojaย kuhamishwa kwenda Nchi nyingine au kuonywa”ย
“Kwa vyovyote Rais ni mhusika nambari moja wa Matukio yote,ย hajui kama ninafanya kazi na Dawson” Alieleza Zolaย
“Safi sana! Mchezo umeisha hapo, soma kauli yake kishaย jiongeze Zola….Kifo chako kinaweza kutokea leo baada yaย kukoswa sana Miaka mingi tulipokuwa tukifanya Operesheniย Upepo, ulikuwa Simba usiyejulikana unayelipigania Taifa lako,ย Dawson anahitaji pongezi kwa kuwaficha Askari tunao tumikaย kwenye idara kwa siri sana vinginevyo tungekuwa tunakufa kamaย Kuku huku tukizungukwa na siasa Chafu” Ilikuwa ni sauti yaย Sande Olise akizungumza kwa unakini mkubwa.ย
“Kama Maisha yangu yatakoma leo Ikulu, Sande uje kufanya hiiย kazi kuliokoa Taifa mara moja” Alisema Zola kisha choziย lilimtoka, akakata simu hiyo. Visa vya baadhi ya Askariย kupotea vilikuwa vingi katika Taifa hilo, Zola baada ya Masaaย mawili alikuwa akikaguliwa kwa ajili ya kuingia Ikulu,ย ilikuwa ni mara ya kwanza Zola kuitwa na Rais huyo, si Raisย huyu Pekee bali Zola hakupata kujulikana na Rais yeyoteย aliyepita, hii ilimpa shaka sana Zola kwanini Rais ampigieย simu wakati ambao alikuwa akimbana yule Askari amwambieย ukweli kuwa Nani anafanya Mauwaji yale.ย Comments zikiwa nyingi naachia ya 7 leoleo
Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA SABAย USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kupiga Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย
ย Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx ย Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx ย Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx ย Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx
43 Comments
Inazid kuwร ya moto
Admin leta no 7 kabisaaa
Aisee ni ya moto balaa, admin big up!
Riwaya tamu mno
Oyaaaa Hii Kali Sana Kaka๐ฅ๐ฅleta ya saba leoleo tuendleee ku-enjoy KIJIWENI
Mkuuu ni kali balaaa aseee ww wa dunia ingineeeee
Aaa adimin tuma chengne bx mana tamu san iih story
Achia bampa
Aiseee unajua ku2shika.hii story balaaaa
Admin lete kituu ..stor imefkia patamu kabisa
๐คฃ๐คฃ๐คฃ 7,8 alooooh!!! Hauchoki kusomaa
Aloohh matukio yamepangiliwa vizurii sanaa….hongera mwandishi
Drop!! Drop it bro!!!
โ๏ธโ๏ธ
Story nzuri sana hii, hongera sana Mtunzi
Utamu kunoga
Safi tunaomba ya Saba
Achia Mzee baba tutililike nayooo
Achia kitu iyomzeebaba turuke nayo
Nakubbal mamb ni moto ๐ฅ๐ฅ
Admin usizingue sas
Nzuri mno jaman
Admin eeh ya 7
watu tumejitoa๐๐
Duu I like to read books like that one โโโโโ
Nilisoma hii story naona kama muv mubasharaaa leta ya 7
Adimn achia mzigo wa 7 huo twende kati duuh
Mzigo wa moto
Imefikia pazur sana…admin achia ya 7 leo tafadhali
ni tamu
Kaliii sanaaa hiyoo blood
Imekaa poa sana
Achia mpaka ya kumi
๐ฅ
Achia kamanda
Comenti nyingi kabisa fanya kweli admin
Achia chuma cha 7
Daaaaa ni balaaa yaani nasoma sitamani iishe inazidi kunoga
Admin umetisha
Motoooo
Actually siasa sio kitu Cha kuingilia pili kuna mambo ukiona sio size yako usiyafanye kwa mfano Zola Leo kaitwa hatujui Nini kina mkuta huko
Achia tu ya saba mkuu
Imekaa poa sanaaaa
Jamani ZOLA