“Ilipoishia” Roho ya Elizabeth ilifukuta kwa maumivu Makali sana, hapo alipaswa kufanya kazi mbili, moja ni kumwokoa MUHONZI Kutoka mikononi mwa mwenyekiti wa chama cha Upinzani na pili alipaswa kutoisalimisha ile flash Muhimu aliyoificha kwenye chupi yake.
Dakika Moja walizungukwa kila upande โMikono juuโ ilisema sauti komavu iliyojaa hasira, ilikua ni sauti ya Brigedia Antony, kila upande walizungukwa na kikosi kazi, Hatimaye Elizabeth aliamini ameshafikia mwisho baada ya siku Tatu za Hekaheka nzito.ย Endelea MSALA SEASON 3ย
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
Chozi liliendelea kumbubujika Elizabeth, alishakiona kifo mbele yake, mwili wa Msichanaย huyu ulitweta ghafla. Alikosa nguvu, Moyoni alimwona Mzee Kimaro kama Msaliti, alionaย Mzee huyo hakupaswa kujisalimisha kirahisi vile, Uamuzi ule ndiyo ukapelekeaย Makomandoo kuzidi kuwazunguka kila kona.ย ย
Brigedia Antony alikua wa kwanza kusogea hapo akiwa na Bunduki yake mkononi,ย alishachoka dharau na kebehi za Bi. Sandra, alijawa na hasira. Alilizunguka Jiwe naย kuwakuta Mzee Kimaro pamoja na Elizabeth wakiwa wameketi. Macho ya Brigedia Antonyย hayakutulia, kwanza alistaajabu kumwona Msichana mwenyewe, alikua Mdogo siyo waย kuwasunbua kwa Muda wote huo, pili ni Mtu aliyekua akimsaidia Msichana huyo,ย alimtazama kama Mzee Goigoi asiyeweza lolote.ย
Akachuchumaa akimkodolea macho Elizabeth, mara akaja Komandoo mmoja kabla hataย Brigedia Antony Kesi hajasema chochote.ย
โTuna maagizo ya kumchukua sasa hiviโ alisema Komandoo huyo aliyemsimamia Brigediaย Antony kwa nyuma, Brigedia alipogeuka alikutana naye uso kwa uso, mazungumzo yalikuaย yakifanyika kwa sauti kubwa kwasababu ya kelele ya panga boi za Helkopta zilizotanda juu.ย
Brigedia Antony hakua na sauti, akasimama ili Elizabeth achukuliwe japo aliona kamaย amedharaulika mbele ya wanajeshi wengine lakini alijua maelekezo hayo yalitoka Ikulu kwaย Rais, hakuna aliyekua na taarifa kua tayari Rais aliuawa.ย
Makomandoo waliwaswamba Mzee Kimaro na Elizabeth ili wawaingize kwenye Helkopta,ย Elizabeth akaweka ngumu baada ya kusimama mbele ya Brigedia kisha akamwambiaย
โUnafanya kosa kubwa sana, utalijutia siku mojaโ baada ya kusema hivyo alisukumwa kwaย nguvu kuelekea kwenye Helkopta, Hatimaye Elizabeth na Mzee Kimaro walinaswa. Taarifaย ya kunaswa kwao ilifika Ikulu kwa Waziri Mkuu Haji Babi mwenye tamaa na Madaraka,ย nyuso za Tabasamu ziliwajaa.ย
Dakika moja, Helkopta zilianza kuondoka eneo hilo la mpaka wa Kiluvya, Uelekeo ukawa niย Black Site kupitia Msitu wa Magoroto Mkoani Tanga, mahali ilipo Black Site ni siri nzitoย sana. Mara moja wakapigwa na kupoteza fahamu ili wasijuwe wanapopelekwa.ย
**ย
Gari nyeusi isiyo na namba ya Usajili iliyokua ikitumiwa na Zagamba ilifika eneo laย Godauni, mshale wa saa yake ulikua ukisoma saa 11:15 Alfajiri, Dakika kadhaa baada yaย
tukio la kunaswa kwa Elizabeth. Uso wake ulijawa na Hasira sana, akaelekea kwenyeย chumba alichohifadhiwa Muhonzi.ย
โUnasikia wewe Mshenzi, Elizabeth amenaswa Muda mchache uliopitaโ alisema Zagambaย akiongea kwa hasira kisha akamwonesha video ya kunaswa kwa Elizabeth, moja ya Askariย walio eneo la tukio walimtumia video hiyo kwa siri sana. Muhonzi alishtuka sana,ย alichokiona kilimduwaza, akajikuta akipepesa macho yake kama fundi saa aliyepoteza nati.ย
Hakujua aseme nini, mikono yake ilifungwa kwa nyuma hivyo hakuweza hata kunyanyuaย chochote. Alijitingisha lakini hakuweza hata kusogea, mara akavutwa kwa nguvuย
โSema ni wapi ilipo M21!โ Alingโaka Zagamba akilihitaji faili la siri la Rais Lucas Mbelwa,ย Mara simu ya Zagamba iliita, alimkata jicho kali Muhonzi wakati anaitoa simu yakeย mfukoni. Kisha aliondoka eneo hilo kwa ajili ya kuzungumza na Simuย
**ย ย
Jua lilikua tayari limeshatua, palionekana kua na hali ya kawaida sana siku hiyo lakiniย palikua na siri nzito juu ya kifo cha Rais Mbelwa, Waziri Mkuu Haji Babi na washirika wakeย walifanya kikao cha siri ndani ya Ikulu, kikao hicho kilikua na ajenda kuu moja, ni jinsi ganiย watafanya mapinduzi baada ya kifo cha Rais Mbelwa, kitu cha kwanza walichokipaย kipaumbele ni nyaraka M21 ambayo ilikua na siri nyingi za Rais Mbelwa na baadhi yaย viongozi wengine wa ngazi za juu akiwemo Bi. Sandra ambaye alikua Mshirika mkubwa waย Rais Mbelwa, hata yeye Waziri Mkuu kuna siri zilikuwamo ndani ya Nyaraka hiyo kumhusu.ย
Jukumu la kupatikana kwa nyaraka akakabidhiwa Bi. Sandra ambaye aliaminika kua ni Mtuย hatari sana, akaondoka Ikulu asubuhi hiyo kwa Helkopta tayari kuelekea Kitengo nyeti chaย Black Site.ย
**ย
Jua lilikua linawaka kwa wastani, asubuhi tulivu ilimkuta Benjamin Kingai akiwa ameketiย juu ya jiwe moja ndani ya Msitu wa Magoroto, mazingira hayo yalimfanya Benjamin ajisikieย vizuri, mbele yake palikua na bwawa dogo ambalo alikua akilitupia vijiwe vidogo vidogoย ambavyo vilikua vinatoa sauti nzuri vinapoingia ndani ya Maji.ย
Mara alikuja Malkia Zandawe na kuketi kando ya Benjamin, hakua na hofu tena na Bintiย huyo baada ya kuona mambo makubwa ambayo Binti huyo aliyafanya.ย ย
โUnajisikiaje?โ aliuliza Zandawe akiwa ni mwenye kutabasamu, Benjamin naye aliachiaย tabasamu lisilo na uhakika wa kipi anachokifurahia, akamjibu Malkia Zandaweย
โVizuri, nipo ndani ya Msitu wakoโ kisha alisindikiza kauli yake na kicheko kidogo, akatupaย tena vijiwe ndani ya bwawa.ย
โUsiwe na wasiwasi Benjamin, utaondoka ndani ya Msitu muda siyo mrefu, kwasasa angaliaย zaidi kuhusu hatma ya Maisha yako baada ya kutoka hapaโ akasema Malkia Zandawe hukuย naye akitupa vijiwe, wakaufanya huo kua ni mchezo kwao.
โAsante kwa kusaidia Maisha yangu, sijui bila kunisaidia ningekua wapi sasa hivi, pengineย ningekua nimeshauawa.โ Akasema Benjamin akiwa analengwa na choziย
โUnafikiri ni kwanini huyo Msichana alikua na hizo nyaraka? Na hizo nyaraka zinahusu niniย hasa?โ akahoji Malikia Zandawe akiwa anamtolea macho zaidi Benjaminย
โInaonekana kuna taarifa za siri sana kumhusu Rais, lakini sijui kwa hakika zaidi ni kwaniniย aliziibaโย ย
โBasi huyo Msichana kama atakua hai basi atakua sehemu ya hatari zaidi, kwa Msako uleย sidhani kama atapata mahali pa Kujifichaโ akasema Malkia Zandaweย
โLakini yule Msichana anaonekana kua zaidi ya Msichana, si Mtu wa kawaida. Ana mamboย mengi ya siri anayoyaficha, kingine ni mjuzi wa mbinu za kivitaโ alisema, pakawa na ukimyaย wa kutosha kisha Zandawe akatupa swali lingineย
โUmewaza kuhusu Hatma ya Mtoto wako na mpenzi wako, nyuma yako kuna niniย kitawakuta?โ swali hili lilimpa nyakati ngumu Benjamin, akashindwa kulizuia choziย likamtoka likashuka hadi kwenye mashavu yake Madogo.ย
โKuwaza hatma yao ni sawa na kusema hakuna kifo, nachelea kusema pengineย wameshauawa huko waliko, roho yangu inanisuta ni kwanini niliwakimbia, nilikua mbinafsiย nikasalimisha Maisha yangu bila kuangalia ni Jambo gani litawafikaโ Alipoimaliza hii kauliย aliangusha kilio Benjamin, Malkia Zandawe akajawa na huzuni sana akamwambia Benjaminย
โHata ukilia kwasasa haitokua na Msaada, kikubwa ni kujua ni wapi walipo, na je wapo hai?โย ย
โKujua walipo ni jambo gumu sana, ile sehemu ni hatari, ni sehemu ya siri sana. Ni ngumuย kujua nini kimewafika, naweza kusema wameshakufaโ akasema Benjamin kisha akajiinamia.ย
โNitalichunguza hilo Benjamin, subiriaโ akasema Malkia Zandawe kisha akatoka spidiย kuzama Msituni, Benjamin hakuelewa ni kitu gani kilimfanya Zandawe azame Msitumi kwaย kasi namna ile.ย
Msichana Zandawe, alizidi kukimbia hadi alipofika eneo la Bwawa, hapo aliangaza huku naย kule, eneo hilo ndilo ambalo Benjamin alikua amejitupa Siku ile kwa lengo la kuokoa Maishaย yake kutoka juu ya Helkopta ya Kijeshi.ย
Akasogea hadi chini ya Mti mmoja, hapo chini aliziona kamba ambazo alifungwa nazoย Benjamin, kisha akazichukua kamba hizo akakimbia kurudi alipomwacha Benjamin, alikuaย msichana wa Msituni anayeutawala Msitu huo hatari unaowasumbua wengiย
Alifika alipomwacha Benjamin akiwa anahema sana, kisha akamwonesha Benjamin zileย kamba, haraka Benjamin akazikumbuka, akashuka kutoka juu ya jiwe hadi aliposimamaย Zandawe.ย
โUnataka kufanya nini?โ
โSubiria uoneโ akasema Zandawe kisha akapiga mluzi mkali, ghafla ikasikika sauti ya ndegeย mmoja akija walipo, ndege huyo alikua mweupe anayefanana na njiwa mzuri wa kufugwa,ย alipofika hapo alitua juu ya jiwe ambao Benjamin alilikalia muda mchache ulio pitaย
โHuyu ni rafiki yangu anaitwa Gola, ni mpelelezi mzuri anayenipa taarifa nyingi kuhusu haliย ya Msitu, nataka kumtumaโ alisema Malkia Zandawe, kila alichokisema kilikua kama ndotoย kwa Benjamin, alijikuta akitabasamu.ย
Mambo kama hayo aliyasoma kwenye kitabu, ni Mfalme Suleiman pekee ndiye aliyekua anaย uwezo wa kuzungumza na ndege lakini Msichana Zandawe alikua na uwezo kama ule waย kuzungumza na ndege.ย
โUmtume wapi?โย ย
โHuko mahala pa siri, nataka kupajua. Nataka kujua hatma ya Familia yako Benjaminโย alisema Malkia Zandawe kisha alimsogelea ndege Gola, akazungumza naye kwa lugha zaย ndege kisha akampatia ile kamba kama alama ya wapi ilipo Black Site. Kisha ndege huyoย akaruka kwa spidi, akiwa ameishikilia ile kamba mguuni.ย
โGola ataleta majibu ni wapi ilipo Black Siteโ akasema Malkia Zandawe kisha akampaย tabasamu zito Benjamin ambaye alijawa na Bumbuwazi zito, midomo yake ikawa mizitoย kiasi kwamba hakuweza kusema chochote.ย Nini Kitaendelea?
Usikose sehemu ya ishirini na mbili ya MSALA SEASON 3 Kujua kama Elizabeth alipona kwenye Msala huu
Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost MSALA Hapa Kijiweni
Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOMย ย
SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
MSALA xx MSALAxx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA
11 Comments
Kubabeki๐๐.
Mwandishi upewe maua yako..๐ฅ๐ฅ
Hii story unaisoma huku unaiona movie. Mungu azidishe kipaji chako.
wa kwanza kuisoma
Watu kusoma
Mambo hayo moto ๐ฅ๐ฅ๐ฅ
๐ฅ๐ฅ๐ฅ
๐๐๐๐๐
bonge moja la story ningekuwa muigizaji ningeandaa movie
Hakika mwandishi unatuleteaga story kali lakini hii ni zaidi ya story kali hongera sana admin mungu akupe maisha marefu
Story inanikumbusha vitu vingi na venye nasoma Kwa picha
Ni ๐ฅ๐ฅ๐ฅ๐ฅ๐บ kongole adimini mkeka ukitiki hii msala ni kali mno..utakula 3k